MAKARANI WA SENSA MAKETE WAASWA


Mkuu wa wilaya Makete, Josephine Matiro

Na Edwin Moshi, Makete

Makarani watakaoshiriki zoezi la sensa ya watu na makazi wilayani Makete wametakiwa kutenda kazi hiyo kwa moyo na uaminifu mkubwa kama mafunzo yanavyosema ili taarifa zinazohitajika na serikali kupitia zoezi hilo la sensa ziweze kufanikiwa

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya makarani wa sensa yaliyoendeshwa kwa muda wa wiki mbili wilayani Makete, mkuu wa wilaya hiyo Josephine Matiro amesema anaamini makarani hao walipatiwa mafunzo yao ipasavyo kama alivyoshuhudia wakati alivyokuwa akihudhuria wakati wakipatiwa mafunzo hayo na kusema wao wanategemewa kwa kiasi kikubwa kufanikisha zoezi hilo

Amesema endapo watakiuka mafunzo waliyopatiwa kutapelekea zoezi hilo kutofanikiwa hali ambayo haitegemewi na yeye pamoja na serikali kwa ujumla hivyo wanatakiwa kutambua dhamana waliyokabidhiwa ni kubwa hivyo ni azima waifanye kama inavyotakiwa

Pia amewataka kupambana na changamoto zitakazojitokeza na kuhakikisha wanatoa taarifa mapema kwa wasimamizi wao mara moja pindi wanapokutana na changamoto ili ziweze kutatuliwa haraka na zoezi la sensa liendelee

Kwa upande wao makarani hao wamesema wanashukuru kwa mafunzo waliyopatiwa na wameahidi kuekeleza jukumu la sensa lililopo mbele yao kwani wanatambua dhamana waliyokabidhiwa hivyo wamemuahidi mkuu wa wilaya kuwa watafanikisha zoezi hilo kama inavyotegemewa na serikali

Zoezi la sensa ya watu na makazi litatekelezwa nchi nzima kuanzia usiku wa 25/08/2012 kuamkia Agosti 26, mwaka huu hivyo wananchi wote wanaombwa kushiriki zoezi hilo kikamilifu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo