MADIWANI MUSOMA WAIKATAA TAARIFA YA UGAWAJI VOCHA ZA PEMBEJEO ZA RUZUKU

 MUSOMA
 
BARAZA la madiwani limeikataa kupokea taarifa za upokeaji na ugawaji wa vocha za ruzuku za pembejeo za kilimo zenye thamani ya zaidi ya milioni 370 baada ya kubaini kuwa hakuna pembejeo ambazo zimewahi kufikishwa kwa wakulima wa halmashauri hiyo katika msimu wa kilimo wa mwaka 2011/2012.
 
Uamuzi huyo umefikiwa katika kikao cha kawaida cha baraza la madiwani chini mwenyekiti wake Bw Magina Magesa,ambapo kwa pamoja madiwani hao baada ya kukataa  taarifa hiyo wameunda tume ya watu sita ili kuchunguza tuhuma hizo.
           
Wakizungumza kabla ya kuundwa kwa tume hiyo,baadhi ya madiwani hao bila kujali itikadi za vyama vyao,wamedai kuwa hakuna hata kijiji kimoja cha halmashauri hiyo kilichowahi kupokea pembejeo hizo za kilimo kama taarifa hiyo ilivyonyesha huku ikitaja kuwa ununuzi wa pembejeo hizo umeigharimu serikali kiasi hicho cha fedha.
 
Akizungumza katika kikao hicho,mwenyekiti wa halmashauri hiyo Bw Magina Magesa,amesema kitendo ambacho kimefanywa na idara ya kilimo katika kitengo cha vocha za ruzuku za pembejeo,licha ya kuwa ni cha hujuma kubwa kwa wakulima,maendeleo ya halmashauri hiyo pia kitafanya wananchi kukichukia chama cha mapinduzi na serikali yake endapo hatua za kisheria hazitachukuliwa dhidi ya wahusika baada tume hiyo kuwasilisha taarifa yake.
                      
Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Tupa,alibaini baadhi ya halmashauri katika mkoa wa Mara kutumia vibaya vocha za pembejeo za ruzuku zingine zikiuzwa nje ya nchi huku wakitumia wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari kusaini katika vitabu maalum vya kupokelea vocha hizo kwa kuwafanya ni wakulima ambao walistahili mgao huo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo