ELCT MAKETE YAWAASA WANANCHI KUTOTEGEMEA WAHISANI


NA RIZIKI BONZUMA, MAKETE

Vikundi vya kuweka na kukopa wilayani Makete vimeshauriwa kutobweteka na misaada kutoka kwa wa hisani mbalimbali, badala yake wajitoe kwa kuchangia  fedha na vitu mbalimbali kwa ajili ya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu wilayani hapa

Akiongoza harambee ya kuchangia misaada mbalimbali  katika kijiji cha Isapulano wilayani Makete mratibu wa mradi wa pamoja tuwalee unaotekelezwa na shirikal la ELCT Makete Mchungaji Ezekiel Sanga amesema ni wakati sasa wa wanamakete kujitoa wenyewe kusaidia watoto waishio katika mazingira magumu lengo likiwa ni kusaidia watoto hao kutokosa haki zao za msingi ikiwemo malazi elimu na chakula

Aidha katika harambee hiyo iliyosimamiwa na shirika hilo zimepatika  fedha taslimu Tsh 80,000 na zaidi ya debe 8 za mahindi  ambazo zitagawiwa kwa watoto kumi na saba waishio katika mazingira magumu kutoka katika kijiji hicho cha Isapulano

Kwa upande wa wananchi wakijiji hicho wameonekana kufurahishwa na na kitendo hicho na kuongeza kuwa kisishie Isapulano tu bali kiendelee hata sehemu zingine za ndani na nje ya wilaya ya Makete na kuomba watu wenye uwezo kujitoa ili kusaidia watoto hao kwani kwa kufanya hivyo Mungu atawazidishia zaidi ya kile walicho nacho
   


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo