WANANCHI WASHAURIWA KUTUMIA MSIMU WA MVUA KWA AJILI YA SHUGHULI ZA KILIMO

 
WANANCHI Wilayani Tarime mkoani Mara,wameombwa kutumia misimu miwili ya mvua katika wilaya hiyo kulima mazao mbalimbali yakiwemo ya biashara kwa ajili ya kupambana na umasikini.
 
Afisa kilimo wa Wilaya ya Tarime Bw Selvanus Gwiboha,amesema wilaya ya Tarime ina uhakika wa kulima na kuvuna chakula kwa mwaka kutokana na kuwa ardhi yenye rutuba ya kutosha lakini wananchi wake hawaitumia kwaajili ya kuongeza uzalishaji mazao ya kchakula na biashara.
 
Amesema katika msimu huu wa masika Wilaya hiyo inatarajia kuvuna tani 180,106 ambacho kitatosha na kubaki hadi msimu wa vuli utakaoanza Septemba 2012 hadi Januari 2013.
 
Amesema wilayani hiyo ina eneo linalofaa kwa kilimo ni la zaidi hekta 790,630 ambapo eneo linalolimwa ni hekta 69,155 sawa na asilimia 76.30 eneo linalofaa kwa kilimo.
 
Hata hivyo afisa kilimo huyo amesema wilaya imepokeaji na kusambazaji wa vocha za pembejeo jumla za bilioni 1.296 kwaajili ya tani 18,000 za kutosheleza wakulima 18,000 sawa na ekari 18,000,mbolea tani 18,000,Urea tani 18,000 na mahindi chotara tani 18,000 pia jumla ya vijiji 89 vimenufaika na ruzuku za pembe jeo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo