MWANAMKE AJIFUNGUA MTOTO MWENYE VICHWA VIWILI

BUNDA
  
MWANAMKE mmoja Bi Sarah Abidenego mkazi wa mtaa wa Chiringe  katika mamlaka ya mji mdogo wa Bunda mkoani Mara,amejifungua mtoto akiwa na vichwa viwili.
 
Akizungumza katika wodi ya wazazi  katika hosptali ya teule ya DDH iliyoko mjini Bunda mama huyo amesema kuwa  alipokuwa mjamzito alikuwa akisumbuliwa sana na maumivu ya mgongo na kwamba ilipofika siku ya kujifungua  juzi julai 24 alikwenda katika hosptali hiyo kwa ajili ya kujifungua.
 
Amesema baada ya  kufika hospitalini hapo alipokelewa na kupelekwa katika wodi ya wazazi na kwamba ilipofika majira ya  3.45 abuhi alijifungua  mtoto huyo ambaye alikuwa na jinsi ya kike huku akiwa na vichwa viwili.
 
Akielezea suala hilo muuguzi wa zamu katika wodi hiyo ,Bi Sophaleti Majanjala,amesema kuwa mtoto huyo alizaliwa akiwa na uzito wa kilo 1.9   na kwamba  baada ya kuzaliwa alikaa muda wa saa moja na baadaye alifariki dunia.

Hata hivyo mama huyo amemshukuru mungu kwa kuwa ndiye aliyempa kiumbe hicho na pia ndiye aliyekichukuwa kwa hivyo  ana matumaini kuwa iko siku atabeba mimba na atazaa mtoto aliye na viungo kamili kwani hiyo ni mimba yake ya kwanza.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo