SERIKALI YAWATAKA WATUMISHI WATAKAOSHINDWA KUFANYA KAZI ZA SERIKALI KUACHA KAZI!

BUNDA

Serikali wilayani Bunda mkoani Mara imewataka  watumishi wa wilayani humo watakaoshindwa kutekeleza kazi za Serikali kuacha kazi kwa hiari kabla hawajachukuliwa hatua kali za kisheria.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya hiyo Bw Joshua Mirumbe katika mkutano wa hadahara katika kijiji cha Nansimo katika mwendelezo wa ziara yake ya kujitambulisha kwa wananchi wilayani humo.

Katika mkutano huo mkuu wa wilaya huyo alimewaeleza wananchi kuwa mipango mingi ya Serikali haifanikiwi kutokana na baadhi ya maofisa kukaa maofisini na kushindwa kwenda vijijini jambo linalosababisha wananchi kukata tamaa na kuongezeka kwa umaskini.

Mkuu huyo wa wilaya ametumia nafasi hiyo kuwaonya watumishi wote wilayani humo na kamwe hatowavumilia watumishi  watakaoshindwa kutimiza  wajibu wao.

Mbali na kutoa angalizo hilo kwa watumishi wa serikali wilayani humo,Mkuu huyo wa wilaya amewataka wazazi kuwasomesha watoto wao ili taifa lipate wataalam wengi wa fani mbalimbali.
 
Na Augustine Mgendi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo