Dodoma
Waziri mkuu Mizengo Pinda amewataka wananchi na wanasiasa kufuata sheria kanuni na taratibu za nchi ili kudumisha amani na utulivu
Waziri mkuu Pinda ametoa kauli hiyo wakati akiwasilisha makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu bungeni mjini Dodoma na kusema pia kufuatwa kwa sheria na kanuni zitasaidia kudumisha amani iliyopo hivi sasa
Hali kadhalika waziri mkuu amezungumzia pato la taifa pamoja na mikakati ya kukabiliana na ongezeko la ajali za barabarani
WAKATI HUO HUO
Naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Philip Mulugo amekiri kuwepo kwa upungufu wa waalimu katika shule za msingi na sekondari hapa nchini
Katika hatua nyingine naibu waziri Mulugo pia akatoa ufafanuzi akisaidiwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Utumishi Selina Kombani kuhusu mishahara ya waalimu 500 ambao wanadaiwa hawajalipwa, na kusema kuwa si kweli ila ni waalimu 210 ambao hawajalipwa na hii imetokana na taarifa zao kuchelewa kutumwa wizarani
Waziri mkuu Mizengo Pinda amewataka wananchi na wanasiasa kufuata sheria kanuni na taratibu za nchi ili kudumisha amani na utulivu
Waziri mkuu Pinda ametoa kauli hiyo wakati akiwasilisha makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu bungeni mjini Dodoma na kusema pia kufuatwa kwa sheria na kanuni zitasaidia kudumisha amani iliyopo hivi sasa
Hali kadhalika waziri mkuu amezungumzia pato la taifa pamoja na mikakati ya kukabiliana na ongezeko la ajali za barabarani
WAKATI HUO HUO
Naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Philip Mulugo amekiri kuwepo kwa upungufu wa waalimu katika shule za msingi na sekondari hapa nchini
Katika hatua nyingine naibu waziri Mulugo pia akatoa ufafanuzi akisaidiwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Utumishi Selina Kombani kuhusu mishahara ya waalimu 500 ambao wanadaiwa hawajalipwa, na kusema kuwa si kweli ila ni waalimu 210 ambao hawajalipwa na hii imetokana na taarifa zao kuchelewa kutumwa wizarani