Watu 12 wamejeruhiwa baada ya gari waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na gari jingine na kupiduka katika eneo la Mang’oto wilayani Makete
Akizungumza na MTANDAO HUU mkuu wa polisi wilaya ya Makete Bw, Peter Kaiza amesema ajali hiyo imetokea baada ya basi la kampuni ya Penguin lililokuwa likielekea Njombe kugongana uso kwa uso na gari aina ya fuso yenye namba za usajili T 437 BAB
Bw Kaiza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni wembamba wa barabara uliopelekea magari hayo kushindwa kupishana
Aidha amesema kuwa majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika hospitali ya Consolata Ikonda kwa matibabu ambapo majeruhi 7 walitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani na wengine watano bado wanaendelea na matibabu katika hospitali hiyo
Na: Teddy Fabian & Ester John
Akizungumza na MTANDAO HUU mkuu wa polisi wilaya ya Makete Bw, Peter Kaiza amesema ajali hiyo imetokea baada ya basi la kampuni ya Penguin lililokuwa likielekea Njombe kugongana uso kwa uso na gari aina ya fuso yenye namba za usajili T 437 BAB
Bw Kaiza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni wembamba wa barabara uliopelekea magari hayo kushindwa kupishana
Aidha amesema kuwa majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika hospitali ya Consolata Ikonda kwa matibabu ambapo majeruhi 7 walitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani na wengine watano bado wanaendelea na matibabu katika hospitali hiyo
Na: Teddy Fabian & Ester John