Makete
Tatizo la maji lililokuwa likiwakabili wananchi wa vijiji vya Matamba, Ng’onde na Mpangala katika tarafa ya Matamba wilayani Makete sasa litapatiwa ufumbuzi ifikapo mwezi Agosti mwaka huu
Akizungumza na MTANDAO HUU katibu tarafa wa Matamba Bw, Benedict Mwageni amesema tayari mkandarasi kutoka kampuni ya gochi ya jijini Dar es salaam amekwisha wasili na kuanza uchimbaji wa mitaro kwa ajili ya kusambaza mabomba ya maji katika vijiji hivyo
Kwa upande wao wananchi wa vijiji hivyo wamesema kuwa mradi huo ukikamilika utawaondolea adha ya kutembea umbali mrefu na katumia muda mwingi kufuata maji badala ya kufanya shughuli zingine za maendeleo
Aidha wamesema kuwa ujenzi wa mradi huo wa maji utawasaidia kuinua uchumi wao na kuboresha maisha yao kwani muda walikuwa wakiutumia kutafuta maji watafanya mambo ya kimaendeleo na pia wananchi wengine watapata ajira kupitia mradi huo.
Na: Kumbuka Kilando
Tatizo la maji lililokuwa likiwakabili wananchi wa vijiji vya Matamba, Ng’onde na Mpangala katika tarafa ya Matamba wilayani Makete sasa litapatiwa ufumbuzi ifikapo mwezi Agosti mwaka huu
Akizungumza na MTANDAO HUU katibu tarafa wa Matamba Bw, Benedict Mwageni amesema tayari mkandarasi kutoka kampuni ya gochi ya jijini Dar es salaam amekwisha wasili na kuanza uchimbaji wa mitaro kwa ajili ya kusambaza mabomba ya maji katika vijiji hivyo
Kwa upande wao wananchi wa vijiji hivyo wamesema kuwa mradi huo ukikamilika utawaondolea adha ya kutembea umbali mrefu na katumia muda mwingi kufuata maji badala ya kufanya shughuli zingine za maendeleo
Aidha wamesema kuwa ujenzi wa mradi huo wa maji utawasaidia kuinua uchumi wao na kuboresha maisha yao kwani muda walikuwa wakiutumia kutafuta maji watafanya mambo ya kimaendeleo na pia wananchi wengine watapata ajira kupitia mradi huo.
Na: Kumbuka Kilando