Makete
Imebainika kuwa wananchi wilayani makete wakijitolea kujenga shule zao kwa kushirikiana na kamati za shule itasaidia kuinua kiwango cha elimu katika shule zao
Akizungumza na wanahabari wetu ofisini kwake kaimu afisa elimu Bw. Mlowe Leopold amesema kwa hivi sasa serikali haitoi pesa kwa ajili ya kununulia vifaa vya ufundishaji hivyo wananchi wanatakiwa kushirikiana na kamati za shule ili kuweza kuwasaidia waalimu kununua vifaa hivyo kwa ajili ya utendaji kazi
Amesema wananchi wanatakiwa kuwa tayari kuchangia fedha wakati wowote pindi watakapotakiwa kufanya hivyo na kuwaomba viongozi wa kisiasa wilayani hapa kushirikiana na viongozi wengine wa eneo husika ili kuweza kuinua kiwango cha elimu na kuweza kuwapa hamasa katika ujenzi wa shule zao
Ameongeza kuwa wilaya inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na kukabiliwa na waalimu wagonjwa ambao kwa kiasi Fulani liaathiri utendaji kazi na kusababisha huduma ya elimu kushuka kwa kiasi Fulani
Na Raphael Abel/Teddy Fabian/Ester John
Imebainika kuwa wananchi wilayani makete wakijitolea kujenga shule zao kwa kushirikiana na kamati za shule itasaidia kuinua kiwango cha elimu katika shule zao
Akizungumza na wanahabari wetu ofisini kwake kaimu afisa elimu Bw. Mlowe Leopold amesema kwa hivi sasa serikali haitoi pesa kwa ajili ya kununulia vifaa vya ufundishaji hivyo wananchi wanatakiwa kushirikiana na kamati za shule ili kuweza kuwasaidia waalimu kununua vifaa hivyo kwa ajili ya utendaji kazi
Amesema wananchi wanatakiwa kuwa tayari kuchangia fedha wakati wowote pindi watakapotakiwa kufanya hivyo na kuwaomba viongozi wa kisiasa wilayani hapa kushirikiana na viongozi wengine wa eneo husika ili kuweza kuinua kiwango cha elimu na kuweza kuwapa hamasa katika ujenzi wa shule zao
Ameongeza kuwa wilaya inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na kukabiliwa na waalimu wagonjwa ambao kwa kiasi Fulani liaathiri utendaji kazi na kusababisha huduma ya elimu kushuka kwa kiasi Fulani
Na Raphael Abel/Teddy Fabian/Ester John