Mwenyekiti wa CCM Taifa Mh. DKT Jakaya Kikwete
Chama cha mapinduzi (ccm) wilayani Makete kimesema kuwa kimejipanga vyema katika kuhakikisha kinapata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi wa viongozi mbalimbali kwa ngazi ya vijiji na kata wilayani humo
Hayo yamesemwa na katibu wa wilaya wa chama hicho Bw. Miraji Mtaturu wakati alipokuwa akizungumza na wanahabari wa mtandao huu ofisini kwake
Amesema chama chake kimeweka wagombea katika sehemu zote zitakazokuwa na uchaguzi ambapo wanachuana na vyama vingine vya siasa katika baadhi ya vijiji na kwamba kuna baadhi ya vijiji chama hicho kimepita bila kupingwa
Kuhusu kampeni Bwana Mtatiru amesema bado wanaendelea katika sehemu mbalimbali kama Matamba, Ng’onde na Iyoka na kuwaomba wananchi wa maeneo hayo kujitokeza kwa wingi katika kampeni zao ili waweze kusikiliza na kuzielewa ilani za chama hicho
Aidha kufuatia uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 2 mwezi ujao wananchi wameombwa kuzitunza vizuri shahada zao za kupigia kura ili waweze kuitumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura na waweze kumchagua kingozi wanaye mtaka
Na: Tatu Yassin, David Nyembe & Riziki Manfredy
Hayo yamesemwa na katibu wa wilaya wa chama hicho Bw. Miraji Mtaturu wakati alipokuwa akizungumza na wanahabari wa mtandao huu ofisini kwake
Amesema chama chake kimeweka wagombea katika sehemu zote zitakazokuwa na uchaguzi ambapo wanachuana na vyama vingine vya siasa katika baadhi ya vijiji na kwamba kuna baadhi ya vijiji chama hicho kimepita bila kupingwa
Kuhusu kampeni Bwana Mtatiru amesema bado wanaendelea katika sehemu mbalimbali kama Matamba, Ng’onde na Iyoka na kuwaomba wananchi wa maeneo hayo kujitokeza kwa wingi katika kampeni zao ili waweze kusikiliza na kuzielewa ilani za chama hicho
Aidha kufuatia uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 2 mwezi ujao wananchi wameombwa kuzitunza vizuri shahada zao za kupigia kura ili waweze kuitumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura na waweze kumchagua kingozi wanaye mtaka
Na: Tatu Yassin, David Nyembe & Riziki Manfredy