WAZEE WA BANDARI WAIADABISHA SMALL FISH YA TUNDUMA

Nusu fainali ya pili kombe la Tunduma Cup 2012 ilikuwa kati ya wauza simu wazee Bandari FC waliokuwa wakimenyana na na timu ya Mbinde's Fc mchezo uliomalizika kwa wazee wa bandari kuibuka na ushindi wa bao 1-0, bao lawashindi limewekwa kimiani na mchezaji Charles Issa dakika ya kwanza na sekunde ya kwanza

kutokana na ushindi huo timu ya wazee wa bandari watacheza fainali na timu ya wauza dagaa maarufu kwa jina la small fish zote za Tunduma mkoani Mbeya

Fainali hiyo inatazamiwa kupigwa kati ya Jumamosi au Jumapili na itategemea na kamati ya mashindano itakavyokubaliana na mtanangehuo utapigwa  katika dimba la shule ya msingi Tunduma

Na Keneth Ngelesi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo