WANAMAKETE WAOMBWA KUJITOKEZA KUMPOKEA MBUNGE WAO

Katibu wa chama cha mapinduzi CCM wilaya ya Makete Bw. Miraji Ntaturu, amewataka wakazi wa wilaya ya Makete bila kujali itikadi za vyama kujitokeza kwa wingi siku ya Jumatatu, Mei 21 mwaka huu kwa ajili ya mapokezi ya mbunge wa jimbo la Makete (CCM) ambaye pia ni Naibu waziri wa maji Mh. Dkt. Binilith Mahenge, ambaye atawasili jimboni humo

Miraji amesema mapokezi hayo yameandaliwa na chama hicho kufuatia mbunge huyo kuteuliwa na rais Jakaya Kikwete kuwa Naibu Waziri wa Maji, ambapo pia anatarajiwa kuhutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya mabehewani wilayani hapo

Mapokezi hayo ambayo yanatarajiwa kupambwa na pikipiki, viongozi wa vyama na serikali, pamoja na wananchi yataanzia katika mpaka wa wilaya ya Makete na Njombe kuanzia asubuhi, ambapo mbunge anatarajiwa kufika kwenye ofisi za chama hicho kabla ya kwenda kwenye Mkutano wa hadhara


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo