TANZANIA YAPATA FURSA KUWASILISHA MAONI KUHUSU KILIMO

 

 Bi Emelda Taikwa Adam, Afisa Mazingira mwandamizi kutoka Ofisi ya makamu wa Rais Akiwasilisha maoni ya Tanzania katika masuala ya Kilimo na mabadiliko ya Tabia nchi, katika mkutano wa sayansi ya Taaluma ya mabadiliko ya tabia nchi unaendelea mjini Bonn Ujerumani
Tanzania kama nchi nyingine zinazoendelea imepata fursa ya kuwasilisha maoni yake kuhusu kilimo katika kuhimli mabadiliko ya Tabia nchi katika mkutano kimataifa wa 36 wa sayansi na taaluma ya mabadiliko ya tabia nchi, unaendelea mjini Bonn Ujeremani.

Akiwasilisha maoni hayo, katika Mkutano huo Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka Ofisi ya makamu wa Rais Bi Emelda Taikwa Adam ameeleza kuwa, nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zinatakiwa kuangalia zaidi katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi ili kuweza kuongeza uzalishaji na kuhakikisha usalama wa chakula kupitia sekta ya kilimo kwani ndo uti wa mgongo wa Taifa.
            
Bi Emelda aliongeza kuwa, katika kuhimili mabadiliko ya Tabia nchi Tanzania kupitia sekta ya kilimo na tafiti zilizokwisha fanyika kuonyesha kuwa kuna matumizi salama ya mbegu zinazohimili ukame, pamoja na matumizi sahihi ya kilimo cha umwagiliaji, na kuna kila sababu ya matumizi ya teknolojia zaidi ya kisasa na kujenga uwezo kwa wakulima wa kawaida ili kuweza kuhakikisha usalama wa chakula.

Akizungumzia athari za mabadiliko ya Tabia nchi katika sekta ya kilimo bi Emelda amesema kuwa, kupungua kwa mvua kunakopelekea ukame nchini na kuongezeka kwa gesi joto kumeathiri kwa kiasi kikubwa sana sekta ya kilimo, na katika kupunguza gas joto katika kilimo kunahatarisha usalama wa chakula na kupoteza ardhi kwa wenyeji.

Ameongeza kuwa pamoja na kwamba sekta ya kilimo imekuwa na mikakati mbalimbali inayotekelezeka katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, Tanzania inatakiwa kuwa na mfumo ambao utahakikisha kuwa upunguzaji wa gesi joto katika kilimo unatokana na jitihada za kuhimili mbadiliko ya tabia nchi.
kwa hisani ya H@ki ngowi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo