SIMBA YAITANDIKA AL AHLY SHANDY 3-0 UWANJA WA TAIFA

 

 Mchezaji wa timu ya Simba Mganda Emmanuel Okwi akikokota mpira kuelekea goli la timu ya Al Ahly Shandy, huku mchezaji wa timu ya Isaac Seun Malik wa timu ya Al- Shandy ya Sudan akijaribu kumzuia katika mchezo wa kombe la Shirikisho unaofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam Simba, imefanikiwa kuitandika Al Shandy ya Sudan magoli 3-0 katika kipindi cha lala salama na kutoka kifua mbele katika mchezo huo wa kwanza kabla ya ule wa Sudan wiki mbili zijazo.

Magoli ya Simba yamefungwa na wachezaji Patrick Mafisango, Uhuru Selemani na Emmanuel Okwi, hata hivyo mchezji Patrick Mafisango alikosa goli la penati baada ya mchezaji Emmanuel Okwi kuchezewa vibaya na beki wa timu ya Al Ahly Shandy katika kipindi cha kwanza.
 
 Timu zikiingia uwanjani kabla ya mchezo huo kuanza jioni hii.
 Mashabiki wa Simba wakishangilia huku wakiwa wameshika sanamui ya Simba
 Kundi la ushangiliaji la Mpira Pesa kutoka Magomeni likishangilia kwa nguvu
Na Full Shangwe Blog


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo