MRADI WA SHULE SALAMA UNAOENDESHWA NA SUMASESU WAZINDULIWA RASMI NGAZI YA WILAYA HII LEO

Mkurugenzi mtendaji wa SUMASESU Egnatio Mtawa

Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Zainab Kwikwega akiwa na Makamu mwenyekiti wa bodi ya SUMASESU Reuben Mbilinyi

Wajumbe waliohuhuria uzinduzi wa mradi huo


Katibu wa TSD wilaya ya Makete Solomon Ndandu akichangia hoja katika uzinduzi huo

Mkuu wa wilaya ya Makete (aliyesimama) akizungumza na washiriki katika mradi huo


Mradi wa shule salama utakaoendeshwa na shirika la SUMASESU katika shule nne za sekondari wilayani Makete kwa ufadhili wa RFE, umezinduliwa kwa ngazi ya wilaya katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Makete lengo likiwa ni kupambana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanafunzi

Akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa mradi huo  Mkurugunzi wa shirika la SUMASESU Bw. Egnatio Mtawa amesema mradi huo utaendeshwa katika shule nne za sekondari ambazo ni Itamba, Matamba, Mlondwe na Ikuwo pamoja na vijiji jirani vinavyozunguka shule hizo

Bw. Mtawa amezitaja changamoto kubwa walizokutana nazo wakati wa utekelezaji wa programu kama hiyo inayotekelezwa chini ya mradi wa Ujana kuwa ni pamoja na baadhi ya waalimu kukataa kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji, wanafunzi kukatazwa kusema ukweli dhidi ya vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa pamoja na baadhi ya kesi za vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanafunzi kuishia hewani, hali inayokatisha tamaa
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Zainab Ahmad Kwikwega amekemea kitendo kinachofanywa na baadhi ya waalimu wa shule za sekondari wanaokwamisha utekelezaji wa mradi huo kuwa kitendo hicho kinachangia kuporomoka kwa taaluma wilayani hapo na ni kinyume na sheria za nchi

Katika hatua nyingine Mkuu wa jeshi la polisi wilayani Makete SSP Rashid Lundilo ameitaka jamii kutoa ushirikiano wa kutosha pale vitendo vya ubakaji vinavyojitokeza kwa wanafunzi au mtu yeyote kukubali kutoa ushahidi mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake dhidi ya mtuhumiwa

Makamu mwenyekiti wa bodi ya shirika la SUMASESU Bw Reuben Mbilinyi amewataka wadau wote kutoa ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha utekelezaji wa mradi huo



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo