RAIS BINGU WAMUTHARIKA AFARIKI DUNIA

Rais wa Malawi, Bingu wa Mutharika    

Marehemu Bingu wa Mutharika
Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika amefariki dunia mara baada ya kuugua ugonjwa wa moyo

Kifo hicho kimetokea baada ya kukimbizwa hospitali ya mjini Lilongwe mji mkuu wa nchi hiyo baada ya kuanguka ghafla na kuzirai

Hali hiyo ilimpelekea rais Mutharika kuwa mahututi hadi mauti yalipomkuta

Mwanzoni redio ya taifa ilikuwa imetangaza kuwa mutharika mwenye umri wa miaka 78 angelipelekwa Nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi

Taarifa zinasema raisi huyo ilibainika amekwisha fariki dunia muda mchache baada ya kufikishwa hospitalini hapo kwani hali yake ilikuwa mbaya

Kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo makamu wa rais Joyce Banda ndiye anayechukua nafasi ya mkuu wa nchi ingawa kuondolewa kwa banda kutoka chama tawala mwaka 2010 kunaweza kutatiza kipindi cha mpito

Hivi karibuni marehemu Rais Banda alikuwa akituhumiwa kushindwa kuongoza na kutokuendeleza uchumi wa nchi hiyo

Inasemekana alikuwa akimtayarisha mdogo wake Waziri wa mambo ya nje Peter Wamutharika kuwa mrithi wake


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo