KUFUATIA SODA MOJA KUUZWA SH.700, DC MAKETE ATOA TAMKO

Makete             
Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Zainab Ahmad Kwikwega amewataka wafanyabiashara wanaouza soda wilayani Makete kuacha kuuza soda moja sh. 700 na badala yake kuuza bei ya zamani ya sh. 500

Mh Kwikwega ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii na kusema katika msimu huu wa sikukuu ya pasaka wafanyabiashara hao wanatakiwa kuuza soda kwa bei ya  sh. 500 kwa soda moja ili wananchi waweze kusherehekea sikukuu hiyo kwa furaha

Ameongeza kuwa mara baada ya sikukuu ya pasaka kumalizika Afisa biashara wilaya ya Makete atakutana na wafanyabiashara hao kujadiliana kwa pamoja sababu zilizopelekea soda kupanda ghafla na kuuzwa sh. 700 badala ya 500 na mwishowe wawe na azimio la pamoja

Maagizo hayo ya Mkuu wa wilaya yametokea kufuatia wafanyabiashara wilayani hapo kupandisha ghafla bei ya soda kutoka sh. 500 hadi 700 kwa soda moja hali iliyozua manung’uniko miongoni mwa wateja wanaotumia vinywaji hivyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo