DC MAKETE AAGIZA MAJI YALIYOKATWA IWAWA SEKONDARI KWA MIAKA MIWILI KUREJESHWA

MAKETE.
Tatizo  la  maji  lililoikumba  shule  ya  Sekondari  Iwawa  limepatiwa  ufumbuzi  baada  ya  Mkuu  wa Wilaya  ya  MAKETE Mh.ZAINABU  AHMADY  KWIKWEGA Kuagiza  Mamlaka  ya  Maji kuyafungua  maji  yaliyokuwa  yamefungwa  kwa  kipindi  cha miaka miwili Shuleni  hapo.

Akizungumza  na  Uongozi  wa  Mamlaka  ya  Maji Wilaya  ya  Makete  Mh.Kwikwega  amesema Tatizo  la  kukatiwa  Maji  katika Shule ya Sekondari  Iwawa limesababishwa na Kujisahau  kwa  baadhi  ya  Viongozi husika  katika  ulipaji  wa  bili  za Maji  hadi kufikia  kukatiwa  kwa  huduma hiyo   katika  Shule  ya  Sekondari  Iwawa

Aidha  Kaimu Mkuu  wa  Shule  ya  Sekondari  Iwawa Bw FODENI MADYEDYE  amekiri  kutokea  kwa  tatizo  la  Maji  katika  Shule  hiyo  na  kusema  kuwa  kwa  kipindi  cha  miaka  miwili  wanafunzi  wamekuwa  wakitumia  muda mwingi  kwenda kutafuta  Maji nje  ya  eneo  la  Shule  jambo linalopelekea  kukosa  vipindi  na  kushuka  kitaaluma  katika  masomo.

Kwa upande  wake  Meneja wa mamlaka ya Maji Makete mjini Bw, JONASI  NDOMBA  amesema   ni utaratibu  wa   mamlaka  ya  maji  kumkatia mteja  huduma  ya Maji  pindi Mteja  anapo  kuwa  ameshindwa  kulipa ankara  ya  maji  kwa wakati  hukatiwa  Maji  kama hatua  ya  kumkumbusha Mteja kulipa  bili kwa wakati

Kupitia jitihada za Mkuu wa Wilaya  ya  Makete Mh.Kwikwega  kuagiza  Malaka  ya  Maji  kufungua huduma  ya  Maji katika  Shule  ya  Secondari  Iwawa  wanafunzi  pamoja  na familia  za  walimu  wameanza  kunufaika  na  huduma  ya  maji  kupitia  Mamlaka ya  Maji wilaya  pamoja mradi  wa maji  ulio fadhiliwa  na kanisa Katoliki  Makete.

Na:Anitha  Sanga &Aldo  Sanga.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo