WANANCHI WAMAKETE WATAKIWA KUSHIRIKIANA ELIMU

Makete                        
Wananchi wilayani Makete kwa kushirikiana na mashirika mbalimbali ya serikali na yasiyo ya kiserikali yameombwa kuchangia vituo vya elimu ya awali kwa watoto

Hayo yamezungumzwa na Afisa ustawi wa jamii wilayani Makete Bw. Leonce Panga, nakusema kuwa ni muhimu watoto wakapelekwa katika vituo vya kupatia elimu ya awali kabla ya hawajafikia umri wa kuanza elimu ya msingi

Amezitaka serikali za vijiji kuandaa mikakati ya kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na kituo kimoja cha watoto hao wadogo kwa ajili yakufundishwa vitu mbalimbali

Aidha amesema kuwa kuwepo kwa vituo hivyo kutasaidia watoto kuwa na uelewa mzuri wanapoanza elimu ya msingi na walimu kupata urahisi wa kuwafundisha kwa kiwango kilicho bora

Na: Zuhura Sanga & Deo Mgina   


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo