Waumini wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania KKKT dayosisi ya kusini kati wameaswa kuwa na moyo wa upendo na uchamungu hata baada ya kumalizika kwa kipindi cha kwaresma

Hayo yamezungumzwa na askofu mteule wa kanisa hilo Bw,Levis Sanga, ambapo pamoja na mambo mengine amesema kuwa waumini wengi huonesha moyo wa upendo na uchamungu wakati wa kwaresma lakini baada ya kipindi hicho kuisha waumini huacha kabisa mambo hayo jambo ambalo amesema  halimpendezi mungu

Aidha ameeleza kuwa kipindi hiki cha kwaresma ni wakati wa waumini kutubu dhambi zao ili kujiandaa kupokea ufufuo wa yesu kristo ambao unaitwa ushindi wa kristo duniani

Hata hivyo amewataka waumini wenye mali hususani rasilimali mbalimbali kama vipaji na ardhi basi wavitumie kwa usawa

Na:Enesta Ndille,Anitha Sanga, Riziki   Manfred
     


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo