VIJANA WA MAKETE WATAKIWA KUPANDA MITI

Makete                        
Vijana wilayani Makete wametakiwa kuwa na mwamko katika kupanda miti mbalimbali ambayo itawasaidia kwa kujiongezea kipato na kuboresha mazingira pia

Hayo yamesemwa na Afisa misitu wa wilaya ya Makete Bw. Alphibian Sanga alipokuwa akizungumza na mtandao huu nakusema kuwa kwa kufanya hivyo wanaweza kujikwamua kiuchumi wao na taifa kwa ujumla

Bw. Sanga pia amewaomba wananchi kuitumia elimu wanayopewa ya kupanda miti ili kupata mazao mengi itakayowapatia mbao za kutosha kupitia misitu hiyo

Hata hivyo ametoa onyo kwa wale wanaochoma misitu kwa makusudi waache tabia hiyo mara moja na yeyote atakayebainika kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kwenda jela ama kulipa faini isiyopungua milioni moja

Na:Obeth Ngajilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo