DC MAKETE AZURU GEREZA LA WILAYA YA MAKETE

MAKETE

Mkuu  wa   wilaya  ya  Makete  Mh.ZAINABU AHMADY  KWIKWEGA, ametembelea  miradi  ya  ujenzi  wa  nyumba mbili  za  maafisa  wa jeshi la  MAGEREZA, ambazo  zimejengwa  kwa  nguvu  ya Gereza la NDULAMO (w) MAKETE.

Ujenzi  huo  wa  nyumba  mbili  na ukarabati  wa  bweni la  wafungwa umefikiia  hatua  ya  umaliziaji  ambapo mkuu  wa  wilaya  ya  Makete  Mh.KWIKWEGA amtoa  mchango  wake  wa kiasi  cha Tsh. milioni  moja  na laki tatu.

Akizungumza na wafungwa wa gereza la  NDULAMO  Mkuu  wa  wilaya  ya  Makete  Mh. Kwikwega  amekabidhi  cherehani  kwa ajili  ya  wafungwa  pia  amemshukuru mkuu  wa  jeshi  la Magereza Tanzania KAMISHINA JENERALI AUGUSTINO NANYARO kwa  kutoa  ushirikiano  wa kutoa Sare  za  wafungwa  na kuahidi  kujenga  nyumba  moja  kwa ajili  ya  maafisa  wa  jeshi la  Magereza.

Akitoa  shukrani  kwa  mkuu  wa  wilaya  ya  Makete Mkuu wa Gereza la Ndulamo (W) SP. MWAKIJUNGU, ameshukuru  jitihada  za mkuu  wa  wilaya  ya  Makete  katika  kusaidia  baadhi  ya  vifaa alivyotoa  na ujenzi  wa nyumba kwa  maafisa  wa jeshi  la magereza.

SP. MWAKIJUNGU ameongeza  kwa kutoa  taarifa  ya  ujio  wa vifaa  vya gereza  zikiwemo  sare  na  kutambua  jitihada  za  makusudi  za   Mkuu  wa  wilaya  ya  Makete  kutembelea gereza hilo.

Na Aldo Sanga


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo