MCHAKATO WA KATIBA MPYA........

Bagamoyo
Hivi sasa Tanzania ipo katika mchakato wa kuunda  katiba mpya ambapo wananchi na vikundi mbalimbali wamekuwa wakiendesha mikutano na midahalo ili kupata maoni ya wananchi

Katika kutekeleza hayo mtandao wa asasi za kiraia wilayani Bagamoyo mkoani Pwani BANGONET umeendesha midahalo mbalimbali katika jimbo la Bagamoyo na Chalinze kwa lengo la kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kushiriki kutoa maoni katika kuandika katiba mpya

Katibu mtendaji wa BANGONET Leonard Peter amezungumzia baadhi ya maoni yaliyotolewa na wananchi ikiwemo kugundulika kuwa takriban asilimia 10 kati ya asilimia 100 ndio wanaotambua katiba


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo