KERO YA BARABARA HOSPITALI YA WILAYA YA MAKETE

Kufuatia kero iliyokuwa ikiwakera wakazi wengi wanaotumia huduma za kiafya katika hospitali ya wilaya ya Makete kuhusu ubovu wa barabara iendayo hospitalini hapo, suala hilo limetolewa ufafanuzi na uongozi wa hospitali hiyo

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake, kaimu mganga mkuu wilaya ya Makete Boniface Sanga amesema barabara inayolalamikiwa kuwa ni mbovu, sio barabara rasmi ya kuingilia hospitalini hapo, na badala yake barabara rasmi ya kuingilia hospitalini hapo, ni iliyopo njia panda ya Isapulano na Bulongwa eneo la Kona Makete mjini

Ufafanuzi huo umetolewa na kaimu Mganga mkuu huyo kufuatia moja ya msikilizaji wa Kituo hiki kutoa kero yake kuwa barabara inayotumika kwenda hospitalini hapo ni mbovu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo