UKARABATI WA BARABARA UNAHITAJIKA

Moja ya barabara za mitaa zikiwa zimeharibiwa na maji kutokana na mifereji ya kupitishia maji kuziba

Wananchi wametakiwa kushirikiana na serikali kuboresha miundombinu ya barabara za mitaa hasa nyakati za mvua za masika kwani zinakwamisha mambo mengi ya maendeleo katika jamii

Hayo yamezungumzwa na mwenyekiti wa shirika la MASUPHA Benito Chengula katika mahojiano maalum na mwanahabari wetu

Amesema kutokana na uharibifu wa barabara hasa zinazounganisha vijiji mbalimbali wilayani Makete kumeliathiri shirika lao kwa kiasi Fulani kwani wanashindwa kupeleka elimu ya ukimwi kutokana na barabara hizo kutopitika kwa gari kiurahisi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo