ELIMU YA VVU BADO INAHITAJIKA MAKETE

MAKETE

Imebainika kuwa kukosekana kwa elimu ya ukimwi katika jamii wilayani Makete, kunapelekea kuongezeka kwa maabukizi ya mapya ya virusi vya ukimwi wilayani hapo

Hayo yamezungumzwa na mkurugenzi wa shirika la MASUPHA linalojihusisha na watu wanaoishi na vvu wilayani hapo Bi Aida Chengula wakati wa mafunzo ya unyanyasaji wa kijinsia jinsi yanavyopelekea maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi na kuongeza kuwa unyanyasaji huo uanatokana na jamii kukosa elimu ya ujinsia

Aidha amewaomba wawezeshaji haki jamii wa shirika hilo la MASUPHA kuwa na mwitikio mkubwa wa kutoa elimu kwa wanajamii pamoja na kutatua matatizo yao hususan unyanyasaji wa kijinsia

Amesema kuwa huu ni mwanzo wa mradi wao wa kuelimisha jamii lakini wamejipanga kuhakikisha elimu ya unyanyasaji wa kijinsia inawafikia wananchi wote


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo