WALIOSABABISHA MELI KUPATA AJALI WAPANDISHWA KIZIMBANI

Watu tisa wamepandishwa kizimbani huko Zanzibar kwa tuhuma za kusababisha ajali ya meli ya Mv Spice Islander iliyotokea mwezi Septemba 2011 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 200

Moja wa watuhumiwa hao ni Said Abdala aliyekuwa kepten wa meli hiyo ambaye hadi sasa hajulikani alipo lakini naye ni miongoni mwa watuhumiwa

habari zinasema kuwa kila mtuhumiwa ana tuhuma zake na watuhumiwa hao tisa walipandishwa kizimbani kila mmoja kasomewa mashtaka yake na wale ambao hawajulikani walipo nao pia wamesomewa mashtaka yao

Hata hivyo kazi kubwa inayowakabili waendesha mashtaka hao ni kukusanya ushahidi wa kutosha ili kuwatia hatiani watuhumiwa hao na kesi hiyo imeahirishwa na inatarajiwa kusikilizwa tena wiki mbili zijazo kuanzia jana

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na tume iliyoundwa kuchunguza chanzo cha kutokea kwa ajali hiyo inasema ujazaji wa mizigo na abiria kupita kiasi ni moja ya sababu zilizopelekea ajali hiyo kutokea


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo