Mbunge wa jimbo la Momba Condester Sichwale ameshangazwa na hatua ya wabunifu wanaogundua pombe aina ya gongo kubezwa na pombe hiyo kumwagwa badala ya kuungwa mkono kutokana na ubunifu walioufanya
Akizungumza bungeni jijini Dodoma leo Mei 5,2023 wakati akichangia bajeti ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara mbunge huyo amesema haoni sababu ya watu hao kudharauliwa na kubeza ubunifu wao
Mbunge huyo ambaye ametinga bungeni na rundo la chupa za pombe zinazozalishwa ndani na nje ya nchi, amesema nchi inatakiwa iwe na utaratibu wa kuheshimu mawazo ya watu wa chini ambao ndio wazalishaji wa pombe ikiwemo gongo na nyinginezo za kienyeji