Gwajima: Msioe au kuolewa kwa kufuata mkumbo

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dk Dorothy Gwajima amewashauri wanawake na wanaume wasioe au kuolewa kwa kufuata mkumbo.


Dk Gwajima alisema hayo wakati wa kuadhimisha Siku ya Familia Duniani na akihimiza wanaume watimize majukumu yao kama baba kwa vile wao ni kichwa cha familia.

Dk Gwajima amesema watu wasiingie kwenye ndoa kwa sababu ya fulani kaolewa/ kaoa na kwamba kufanya hivyo ni kutengeneza machozi yao wenyewe.

“Niwatie moyo, kwanza tukumbuke tuingie kwenye ndoa kwa mpango, si mtu akitoka yuko na mkewe au mumewe na wewe unaona uingie unasema mimi nitaonekanaje huko ni kujitengenezea machozi mwenyewe,” amesema.

Dk Gwajima amesema mwanaume ama mwanamke anapoingia kwenye ndoa lazima achague rafiki ambao lengo lao ni moja na hapo atakuwa amejipunguzia athari za kuingia kwenye machozi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo