Daktari Feki Atiwa Mbaroni kwa Tuhuma za Kumbaka Mkunga


Polisi katika mji mkuu wa Uganda Kampala wamemkamata kijana mwenye umri wa miaka 18 kwa tuhuma za kumbaka mkunga aliyekuwa akitafuta kazi katika kliniki yake.


Msemaji wa polisi wa Uganda Fred Enanga amewaambia waandishi wa habari kuwa mwanamume huyo alikuwa akijifanya daktari ambaye ana nafasi za ajira katika kituo chake cha matibabu. Enanga amesema mshukiwa huyo alidai kumiliki kituo kisichokuwepo kiitwacho Medical Scrub Uganda na kuwa alitumia ukurasa ghushi wa Facebook na kujiita daktari Ronnie ili kuwalaghai waathiriwa. 


"Angewahoji waathiriwa kwa ufupi mtandaoni na kisha kupanga mkutano ili kujadili sheria na masharti yatakaoongoza uajiri wao," Enanga alinukuliwa katika gazeti la The Daily Monitor.


Mshukiwa anasemekana kuwabaka wanawake hao walipojitokeza kutia saini mikataba ya kazi hizo feki. Mnamo Machi 21, mshukiwa aliripotiwa kumhoji mkunga mwenye umri wa miaka 21 kutoka jiji kuu la Kampala na kisha kumwalika katika kijiji cha Mukono ambapo alimbaka mwathiriwa. "Baada ya uchunguzi wetu tulitumia kikosi cha mafisa wa angani kumsaka mshukiwa huyu ambaye tulifanikiwa kumkamata.


Tumebaini kuwa mshukiwa hakuwa na mahali pamoja pa kufanyia shughuli zake na kuwa alikuwa analala kwenye nyumba za kulala wageni za bei nafuu katika maeneo ya Kayunga na Mukono,” msemaji wa polisi alisema. Mshukiwa anasemekna kutekeleza uhalifu wake katika maeneo ya Kayunga na Mukono ambayo yako kilomita kadhaa kutoka jiji kuu la Kampala. 

Chanzo: TUKO.co.ke 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo