Mwandishi wa TBC afariki dunia akishuka Mlima Kilimanjaro


Mwandishi wa habari na mpiga picha wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) mkoani Manyara Joachim Kapembe amefariki dunia alipokuwa akishuka kutoka katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.


Kapembe pamoja na watendaji wengine wa wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari walipanda kwenye mlima Kilimanjaro tarehe 9 mwezi huu kwa ajili uzinduzi wa intaneti ya mwendokasi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).

Alizaliwa tarehe 26 Februari mwaka 1977 wilayani Muheza mkoani Tanga.

Aliajiriwa na TBC Oktoba Mosi mwaka 2011 kwa cheo cha mpiga picha daraja la II.

Hadi anafariki dunia tarehe 13 mwezi huu alikuwa na cheo cha mpiga picha mkuu daraja la I.

Joachim Kapembe ameacha mke na watoto wawili.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo