Mwanahabari afariki akiripoti Kombe la Dunia


Mwanahabari maarufu wa Marekani, Grant Wahl (48), amefariki dunia wakati akiripoti michuano ya soka la Kombe la Dunia nchini Qatar kati ya Argentina na Uholanzi Desemba 9, 2022.


Wahl, alianguka ghafla wakati alipokuwa akitazama na akiwajibika katika mchezo huo wa Ijumaa usiku huku ripoti za awali zikionesha kuwa alipatwa na mshtuko wa moyo madai ambayo bado hayajathibitishwa.


Aidha, itakumbukwa kuwa Novemba, 2022 Wahl alizuiliwa kwa muda mfupi na mamlaka ya Qatar kwa kujaribu kuingia uwanjani akiwa amevalia shati la upinde wa mvua, kuunga mkono haki za wapenzi wa jinsia moja LGBT.

Shirikisho la Soka la Marekani limesema limesikitswa na tukio la kifo cha Grant aliyekua akituma ujumbe katika ukurasa wake wa Twitter kuhusu mechi ya Uholanzi na Argentina, kabla taarifa ya kifo chake kutangazwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo