Mchungaji awafukuza kanisani waumini walioshindwa kutoa sadaka

Pasta mmoja alikasirishwa sana na waumini wake wengi waliokosa kutoa fungu la kumi na sadaka, kisha kuwaagiza kuinuka na kwenda nyumbani kwa kuzembea kwao kuja kanisani bila sadaka.



Video inaonyesha kwamba waumini wawili wakifika mbele ya madhababu kuweka sadaka zao ndani ya kikapu, kisha pasta huyo akasema maombi mafupi kabla ya kuwaagiza waumini kwenda nyumbani.


"Father we thank you for the offerings today, we appreciate you in Jesus' name. Let's stand up as we go home," pasta huyo aliomba. Pasta huyo aliwakashifu waumini hao kwa kukosa kutoa sadaka.


"You know we will not be joking when it comes to giving. If you don't want to give just go home. I release the blessing as you go home. Enjoy your week in Jesus' name. Amen!" alisema pasta huyo. Pasta huyo alisema hawezi kuwalilia waumini wake kutoa sadaka. "Take those baskets to the office. We are through. Mbarikiwe. You are blessed. I will not beg people in this church to give. I'm not a beggar," mhubiri aliongeza kusema.


Video hiyo ilisambazwa kwenye Twitter na Wamutahi na wafuasi wake walitoa maoni mseto. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo