Amzika mtoto wa wiki mbili akiwa hai ili apate muda wa kujiuza


Mtoto mwenye umri wa wiki mbili amefariki dunia baada ya mama yake aliyefahamika kwa jina la Oliva Meshack, mkazi wa Mtaa Buselesele katika mji mdogo wa Katoro wilaya ya Geita mkoani Geita kumzika akiwa hai.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akieleza kuwa Oliva alifanya kitendo hicho ili apate muda wa kwenda kujiuza.


Baada ya kupata taarifa hiyo Kamanda Safia amesema walifukua eneo kilipozikwa kichanga hicho na kukuta tayari amefariki.


Amesema binti huyo ambaye anashikiliwa na polisi mkoani humo alikuwa pia akiuza baa na aliona mtoto huyo angemzuia kuendelea na biashara yake haramu ya kujiuza.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo