
Video ya bibi harusi aliyeketishwa kwenye paa la daladala imewashangaza watu wengi katika mitandao ya kijamii.
Katika kipande hicho kifupi, bi harusi alikuwa peke yake kwani bwana harusi hakuwepo, lakini watu wengi walimzunguka. Ilionekana kana kwamba basi hilo lilikuwa limepangwa kwa ajili ya kumbeba pekee, lakini jambo la kushangaza ni kwamba alikuwa juu ya paa la gari hilo.
Bibi harusi alionekana kutoshangaa wala kupinga wakati ulipofika wa yeye kupanda basi, na kuwafanya baadhi ya watu kuamini kuwa huenda huo ni utamaduni wao. Hili halijathibitishwa hata hivyo.