Nape aongoza zoezi la kudeki barabara kwa ajili ya Rais Samia

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, ameungana na vijana wa mkoa wa Lindi kufanya usafi maeneo mbalimbali ya mkoa huo ikiwa ni maandalizi ya kumpokea Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye atawasili mkoani humo kesho Desemba Mosi, 2022.


Vijana hao walifanya zoezi hilo la kusafisha barabara baada ya kumaliza matembezi maalum katika maeneo mbalimbali ambapo walitumia fursa hiyo kufikisha salamu zao kwa Rais Samia kupitia kwa Waziri wa Habari Nape.


"Sisi Vijana wa Lindi ilifikia hatua baadhi ya wanasiasa walituita watoto tuliotengwa lakini walisahau licha ya mkoa wa Lindi kutotembelewa na Rais kwa muda mrefu Mama yetu Samia Suluhu akiwa Makamu wa Rais alitutembelea sana" Amesema Mustafa Dumbo kwa niaba ya vijana wa Lindi


Akiwajibu vijana hao Waziri Nape Nnauye amewataka vijana hao kutambua Rais Samia anaupenda sana mkoa wa Lindi na ndiyo maana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, anatokea huko.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo