Leo Novemba 12,2022 wananchi
hao wamefika katika eneo hilo kwa ajili ya kufanya matayarisho ikiwemo kuchimba
visiki na kung'oa miti iliyopo katika eneo hilo tayari kwa maandalizi ya ujenzi
wa zahanati hiyo
Wamesema zahanati hiyo ikikamilika
itawezesha wananchi hao kupata matibabu madogo madogo kwa haraka na kuepuka
kwenda hospitali kupata matibabu hata ya magonjwa ambayo yangeweza kutibika
katika ngazi ya zahanati
Upendo Sanga ni Katibu wa
Kitongoji cha Luchala inapojengwa zahanati hiyo amesema ujenzi huo ameupokea kwa mikono miwili na uhitaji upo licha ya kuwa na hospitali kubwa kijijini hapo
Nancy Swai ni Afisa
Maendeleo ya jamii kata ya Tandala lakini pia ni Kaimu afisa mtendaji wa Kijiji
cha Ikonda amesema mradi huo ni kwa ushirikiano na mfuko wa maendeleo ya jamii
(TASAF) hivyo kuishukuru kwa wao kama kijiji kupata mradi huo
Amesema Kijiji hicho kina
uhitaji wa zahanati kwa sasa hata kama kuna hospitali kwa kuwa sio kila
matibabu yanapatikana katika hospitali kubwa hivyo magonjwa mengine yatatibiwa
katika zahanati yao na pia itasaidia kuokoa muda
Diwani wa kata ya Tandala
Daniel Hatanaka akizungumza eneo la tukio amesema wanaupokea kwa mikono miwili
mradi huo na kuwaomba wananchi kujitokeza kufanya shughuli za maendeleo pale
wanapohitajika kwa kuwa kukamilika kwa zahanati hiyo kwa siku zijazo inaweza
kuja kuwa kituo cha afya







