Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Amini Salum ameuwawa baada ya kupigwa risasi wakati wakiwafukuza watu wanaodaiwa kuwa majambazi waliotaka kumpora mfanyabiashara ambaye jina lake limehifadhiwa.
Tukio hilo limetokea mtaa wa Nyamalembo Mjini Geita majira ya saa sita usiku baadhi ya mashuhuda wamesema walisikia kelele ambapo kwenda kuangalia wakakuta mfanyabiashara kavamiwa na watu wanaodaiwa majambazi na kuamua kutoa msaada wa haraka kwa kuwasaka na wakiwa katika harakati hizo ikasikika mlio wa risasi iliyokwenda kumpata Amini na kusabisha kifo chake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Safia Jongo amekiri kutokea kwa tukio hili na Polisi linaendelea na uchunguzi wake.Auwawa kwa risasi akitoa msaada
Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Amini Salum ameuwawa baada ya kupigwa risasi wakati wakiwafukuza watu wanaodaiwa kuwa majambazi waliotaka kumpora mfanyabiashara ambaye jina lake limehifadhiwa.
Tukio hilo limetokea mtaa wa Nyamalembo Mjini Geita majira ya saa sita usiku baadhi ya mashuhuda wamesema walisikia kelele ambapo kwenda kuangalia wakakuta mfanyabiashara kavamiwa na watu wanaodaiwa majambazi na kuamua kutoa msaada wa haraka kwa kuwasaka na wakiwa katika harakati hizo ikasikika mlio wa risasi iliyokwenda kumpata Amini na kusabisha kifo chake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Safia Jongo amekiri kutokea kwa tukio hili na Polisi linaendelea na uchunguzi wake.
