Afungwa jela maisha kwa kumlawiti mtoto wa miaka 8

Mahakama ya Wilaya ya Iringa imemuhukumu kifungo cha maisha na fidia ya Tsh. Millioni 5 Aalon Mveyange kwa kosa la kumlawiti Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 8 aliyekuwa akisoma darasa la pili katika Shule ya Msingi Mgongo.


Aalon mwenye umri wa miaka 36 alikuwa akijishughulisha na Kilimo amekutwa na hatia na alikuwa anafahamiana na Mtoto huyo kwasababu alikuwa anaishi Jirani yake.

Akisoma Hukumu Hiyo Hakim Mkazi Mkuu Said Ally Mkasiwa amesema Aalon aliwakuta Watoto wakicheza akawatuma kwenda kununua pipi kisha akabaki na Binti huyo na kumpeleka chooni kisha kumuingilia kinyume na maumbile.

Mahakama ilipompa nafasi ya kujitetea Aalon aliiomba Mahakama kumpunguzia adhabu kwasababu ana matatizo ya afya na Mke wake ni mjamzito na muda wowote atajifungua na anategemewa na Familia

Hata hivyo Mahakama ikamuhumu kifungo Cha maisha na fidia ya Tsh. Millioni 5 kwa kosa hilo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo