Afisa akamatwa akiomba rushwa ya shilingi 10,000

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Njombe imemkamata na kumfikisha Mahakamani Rashid Mkocha ambaye ni afisa kilimo wa kata ya Mlowa halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe kwa tuhuma za kumuomba rushwa ya shilingi elfu kumi (10,000) mkulima ili asajiliwe kwenye kitabu kwa ajili ya mbolea ya ruzuku.


Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Njombe Kassim Ephrem amesema mtuhumiwa alikamatwa November 9 mwaka huu mara baada ya kupata taarifa kwa raia mwema na kuandaa mtego uliosaidia kumkamata mtuhumiwa.


“Tumemfungulia kesi afisa kilimo wa kata kwa kudai rushwa kwa mwananchi asajiliwe kwenye kitabu ili aweze kupata namba akachukue mbolea ya ruzuku halafu yeye ni afisa kilimo wa kata hata ukimuangalia mkulia unaona dah”amesema Kassim Ephrem.


Ametoa wito kwa kuacha vitendo hivyo kwa kuwa serikali ina nia njema ya kuwasaidia wananchi hivyo hawataweza kusita kumchukulia sheria mtumishi yeyote anayekwenda kinyume na sheria.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo