Achangisha pesa za mafuta ya "Ambulensi"

Kijana mmoja nchini Ghana alijitwika jukumu la kuchangisha pesa za kuweka mafuta kwenye gari la wagonjwa ili kuliwezesha kusafirisha majeruhi wa ajali ya barabarani waliokuwa mahututi.


Katika video iliyofikia Radio Jambo, kijana huyo alionekana akiwaomba na kuwahamasisha raia waliokuwa wamejumuika kwenye eneo la tukio la ajali kutoa pesa za kujaza tenki ya mafuta ya  Ambulensi hiyo.


Ajali ilitokea wakati gari lililokuwa limebeba nyanya lilianguka na kubingirika. Dereva wa gari hilo aliachwa na majeruhi mengi. Ambulensi lilifika kuwachukua majeruhi lakini la kuhuzunisha ni kuwa gari hilo halikuwa na mafuta na halingeweza kusonga wala kunguruma.


Gari hilo la wagonjwa lilisababisha msongomano mkubwa barabarani huku likishindwa kusonga mbele. Wengi wa waliotazama video hiyo wameeleza kukerwa kwao na suala la ambulensi kukosa mafuta.


Katika video hiyo, wakaazi walighahabishwa na kitendo hicho huku wakiwashtumu wahudumu wa ambulensi kwa kutowajibika.


Kwenye mitandaoni ya kijamii, wanamitandao walieleza kero yao kutokana na kitendo suala hilo. 

Chanzo: radio Jambo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo