"Samatta, Msuva wakatwe miguu ili kushiriki kombe la dunia kwa timu ya wenye ulemavu"

Mtumizi mmoja wa Facebook amewachekesha wanamitandao baada ya kuachia maoni ya utani mno kuhusu timu ya walemavu ya mpira wa miguu Tanzania kufuzu robo fainali ya kombe la dunia.


Shirika la habari la BBC Swahili kupitia ukurasa wao wa Facebook waliripoti taarifa hizo kwamba timu ya taifa ya mpira wa miguu kwa walemavu, Tembo Worriors, ambayo ni ya kandanda ya wanaume imefuzu robo fainali ya kombe la dunia.

“Timu ya taifa ya walemavu ya Tanzania imetinga robo fainali ya kombe la dunia kwa watu wenye ulemavu baada ya kuichapa Japan 3-1 katika mchezo wa hatua ya 16 bora huko Uturuki. Tanzania sasa itakutana na Haiti waliomfunga Marekani 6-2, katika mchezo wa robo fainali utakaopigwa kesho,” BBC waliripoti.

Baada ya taarifa hizi za kufurahisha, haswa ikizingatiwa kuwa Tembo Worriors ndio wawakilishi wa pekee kutoka bara zima la Afrika, wanamitandao walifurika kutolea maoni yao wengine wakiwapongeza ila kuna mmoja aliyezua utani kupitiliza na kufanya maoni yake kuzungumziwa sana mitandaoni.

Mtumizi huyo wa Facebook kwa jina Jackson Boniface alitoa maoni yake kwa kuwapongeza walemavu hao na kuchagiza zaidi kwamba ni wakati sasa baadhi ya wachezaji wenye viungo vyao vyote kwenye timu ya Taifa Stars kukatwa miguu ili kuongeza nguvu kwenye timu hiyo ya walemavu.

“Tuwekeze huko huku, kwa miguu miwili hatuwezi, na ikiwezekana Msuva, Fei Toto na Samata wakatwe mguu mmoja kila mmoja wakaongeze nguvu,” Boniface aliandika.

Baadhi ya watu waliotangamana na maoni haya walichekeshwa na fikira za mwamba huyo.

“Umeongea kama utani lakini kiukweli ndani kuna ujumbe mzito sana TFF wanapaswa kutafuta namna ya kuiboresha Taifa Stars na kupandisha morali ya watanzania, Wakiendelea na huo upendeleo na ubaguzi wa baadhi ya timu tutaendelea kuwa wasindikizaji haileti maana kuona kiongozi ana wasiwasi wa kusuasua kwa timu yetu,” Procesius Rweyendera alimwambia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo