Mama ashtakiwa kwa kumtupa mtoto wake mchanga kwenye mto

Mwanamke mwenye umri wa miaka 22 alishtakiwa Ijumaa kwa kumtupa mtoto wake mchanga kwenye mto Chania kaunti ya Nyeri nchini Kenya


Elsie Makena alikabiliwa na shtaka la kujaribu kuua mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mercyline Lubia.


Mahakama ilisikia kwamba tukio hilo lilitokea mwendo wa saa kumi na mbili jioni siku ya Jumatano.

·

Lakini mvulana huyo mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi saba aliokolewa na msamaria mwema dakika chache baadaye.


“Mtoto huyo amechukuliwa na nyumba ya watoto mjini kwa usalama wake,” ilisema ripoti ya polisi iliyotolewa mahakamani.


Bi Makena alikanusha shtaka hilo na kuomba masharti nafuu ya bondi.


Hakimu Lubia alimpa bondi ya Sh1 milioni na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.


Kesi hiyo itaendelea Novemba 8.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo