Binti wa kazi yamfika, begi lake lakutwa na "ndumba", Bosi wake Acharuka

Flora Juma (18), ambaye amekuwa akifanya kazi za ndani katika familia moja iliyopo mtaa wa Kombo Masai, Kata ya Malolo Mjini Tabora, amejikuta yuko matatani kwa kutuhumiwa na uchawi, baada ya bosi wake kukagua na kukuta begi lake lina dawa za kienyeji.

Mama wa familia ambayo binti huyo amekuwa akifanya kazi za ndani Shamira Ngoma, amesema alianza kupata sintofahamu juu ya binti huyo baada ya siku ya kwanza kumkagua katika begi lake alipofika na kukuta kifurushi cha dawa za kienyeji ambapo binti huyo alimweleza hutumia dawa hizo katika kujitibu maumivu ya tumbo ambayo husumbuka nayo.


Shamira amesema mwenendo wa maisha ya binti nyumbani hapo uliendelea kumchanganya,kwani wakati mwingine alikuwa akifanya vitu kama mtu asiyekuwa na utimamu wa akili, hatua iliyomfanya kufikia uamuzi wa kutaka kumrudisha nyumbani kwao wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo wakati akimwandalia nguo katika begi lake tayari kwa kumsafirisha alikuta tena mchanga na shanga vikiwa vimefungashwa kwenye karatasi.

Kwa upande wake Flora akijibu tuhuma ya ushirikina dhidi yake amesema mchanga na shanga vilivyokutwa ndani  ya begi lake aliagizwa na bibi yake ambaye alimtokea kimazingara usiku wa Oktoba 23 mwaka huu, wakati akiangalia runinga sebuleni na kumwambia achote mchanga nje ya nyumba ya familia hiyo na baadaye ataufata bila yeye kujua utakwenda kufanyiwa kazi gani .

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo wa Komba Masai, Dotto Kitungulu, amefika katika nyumba ya familia hiyo ambapo amehakikisha usalama wa binti huyo ambaye alikuwa amezingirwa na wananchi mpaka aliposafirishwa  kurudi nyumbani kwao mkoani Shinyanga.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo