Leo kulivyo Nyumbani kwa mlezi wa Maria na Consolata

Watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Makete Ngazi ya kata ya Tandala wamefika nyumbani kwa mlezi wa Maria na Consolata kutoa pole kwa msiba wa mapacha hao

Watumishi hao wakiongozwa na Diwani wa kata hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa halmashauri Mh Egnatio Mtawa wamempa pole Mama mlezi wa watoto hao Bi Bertina Mbilinyi na kusema msiba huo umewagusa wote

Wamesema wanatambua mchango wa mama huyo mlezi aliyeishi nao kwa miaka 7 tangu walipoanza darasa la kwanza mpaka darasa la 7 na ndiye aliyewafundisha mambo mengi na bado walikuwa wanamtambua kama mama yao mpaka walipofikwa na umauti

Akitoa salamu za pole kwa niaba ya serikali Mwenyekiti wa Halmashauri Mh Egnatio Mtawa amesema serikali ngazi ya wilaya chini ya Mkuu wa wilaya Mh Veronica Kessy itashirikiana naye mwanzo mpaka mwisho wa msiba huo na kwa sasa inaandaa rambirambi kwa ajili ya kumkabidhi mama huyo mlezi

Kwa upande wake Mama mlezi wa Marehemu Maria na Consolata Bi Bertina Mbilinyi amewashukuru watumishi hao kwenda kumpa pole kwani amejisikia faraja japo msiba huo unampa machungu kwa jinsi alivyoishi na watoto hao muda mrefu

"Nilikwenda kuwatembelea wakiwa wamelazwa hospitali Dar es salaam na sikuwa na kitu cha kuwapa lakini nilipowauliza mnataka niwape nini walisema mama tunataka supu ya kuku" amesema mama huyo mlezi

Amesema kwa sasa anajiandaa kwenda Iringa kwa ajili ya maziko yanayotarajiwa kufanyika Tosamaganga jumatano ya wiki hii


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo