Rapa Stamina na mchumba wake wafunga ndoa (PICHAZZ)

Hatimaye rapa Stamina amefunga ndoa  na mchumba wake wa muda mrefu ajulikanaye kwa jina la Veronica jana Mei 05, 2018 mjini Morogoro katika kanisa la Mtakatifu Consolata lilipo maeneo ya SUA mjini humo.
Stamina na mkewe Veronica wakivishana pete.
Kwenye harusi hiyo, Wasimamizi walikuwa ni swahiba wake Roma Mkatoliki na Mkewe Nancy ni kwa mujibu wa maelezo ya Stamina.
Mwaka jana rapa Stamina alimvisha pete ya uchumba mchumba wake huyo, Bongo5 inawatakia kila la kheri katika maisha yenu mapya ya ndoa.
Tazama baadhi ya picha hapa chini za tukio hilo.
Picha by Clouds Digital


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo