Rais Mstaafu Mkapa, amuibua Mbatia Bungeni

Mbunge wa Jimbo la Vunjo, James Mbatia ameikumbusha serikali ya awamu ya tano makubaliano waliyokubaliana awamu ya tatu adhma ya kujenga chuo cha kitaifa cha kisiasa nchini kitakachoweza kuwaanda viongozi wa kisiasa bila ya kujali itikadi za vyama

Mwaka 2002/04 tulikubaliana kati ya wadau wa vyama vya siasa na serikali tuwe na chuo cha Kitaifa cha kuandaa viongozi bila kuangalia itikadi za vyama kipindi cha Awamu ya Tatu Je, Serikali imefikia wapi katika kuandaa chuo hicho ili tuwe na taifa 1 lenye malengo yanayo fanana?
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde ambaye alijibu kuwa nia na dhamira ya serikali ni kuendelea kukuza demokrasia ndani ya nchini.
“Nia na dhamira ya serikali ni kuendelea kukuza demokrasia ndani ya nchi na makubaliano yaliyofanyika mwaka 2002-2004 tutaendelea kuyafanyia kazi na kufuatilia ili ombi hili liweze kutimia la kuwa na chuo cha kuwaweka wanasiasa. Tunaamini kupitia chuo hicho basi tutakuwa tumejenga taifa la watu wazalendo na wenye ari ya kweli ya kuwatumikia watanzania”, amesema Mavunde.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo