Akitoa tararifa kwa waandishi wa habari Mh. Mahmoud amesema hatua hiyo imelenga kuimarisha imani za watu kwa wanaofunga huku akizitaka manispaa ndani ya Mkoa huo kusimamia agizo hilo.
"Ili waumini waweze kuukabili mwenzi huu kiukamilifu ni lazima kwa wananchi kutumia fursa za ramadhani kwa kufanya mambo mema ili Mwenyezi Mungu aweze kuzikubali swaumu", amesema Mahmoud.
Aidha, Mahmoud amewataka watembezaji watalii kutoa mwongozo kwa wageni kwa kufuata utaratibu ulio sahihi kwa kuvaa mavazi ya heshima na yanayo kubalika kutokana na mila, silka na utamaduni.
Kwa upande mwingine, Mkuu wa Mkoa huyo ameliagiza Jeshi la Polisi kuongeza doria wakati wa jioni ili kuimarisha hali ya ulinzi na usalama wa raia na mali zao sambamba na kuimarisha usalama wa barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima.
