Mhadhiri huyo wa chuo cha biashara katika chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) Rose Mdenye ameuawa kwa kuchomwa kisu na mumewe usiku wa kuamkia leo mei 26 huku sababu ikitajwa kuwa ni wivu wa mapenzi.
Rose Mdenye ameuawa kwa kuchomwa kisu na mumewe wa ndoa ambaye ni mchungaji wa Kanisa aitwaye John Mwaisango.
Tukio hilo limetokea kwenye nyumba yao mjini Dodoma.
Chanzo: mwananchi
Ofisa habari na uhusiano wa chuo kikuu hicho (UDOM), Beatrice Mtenga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na amesema kuwa taarifa zaidi zitatolewa baadae.
Mtenga amesema msiba upo Kisasa Sheli.
